JAMHURI YA MUUNGANO TANZANIA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII
TANGAZO
Katibu Mkuu, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii anapenda kuwatangazia
Wauuguzi wa ngazi ya Astashahada na ngazi ya Stashahada
waliohitimu mafunzo mwaka 2013 wawasilishe maombi ya kupangiwa vituo vya kazi. Waombaji wanatakiwa kupendekeza maeneo matatu wanayotaka wapangiwe kazi.
Maeneo yenye nafasi za kazi yameainishwa kwenye tangazo la kazi
kwenye tovuti ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
(www.moh.go.tz).
Maombi wayawasilishwe kwa
Katibu Mkuu,
Wizara ya Afya na Ustawi waJamii
kwa anuani ya hapa chini kabla ya tarehe 14 Machi, 2014
Katibu Mkuu,
Wizara ya Afya na Ustawi
wa Jamii,
S.L.P. 9083,
DAR ES SALAAM
Share this
0 Comments